Kanisa la Ufunuo Tanzania linapatikana Kimara Bonyokwa ndani ya Jiji la Dar es salaam.
Kwa wale wanaotokea njia ya mjini kwa kutumia Barabara ya Morogoro ukifika Kimara mwisho upande unaoshukia wa kushoto utaona stendi ya bajaji na magari yanayokuja Bonyokwa.
Kwa wale wano tokea njia ya Mbezi mwisho ukishuka Kimara unavuka upande wa pili wa barabara ukipanda hayo magari au bajaji utashuka kituo kwa Bendera Kanisani utakua umefika
Kwa wale wanaotokea stendi ya Segerea panda Bajaji au magari yanayokuja Bonyokwa mwisho ukifika hapo ulizia kwa Bendera utaelekezwa.